News

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali akiwaaga wanafunzi wa Ufadhili wa Masomo nchini Rasilhema

2023-09-09 13:43:29.0

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Ally Abdul Gulam amewataka wanafunzi waliopata bahati ya Ufadhili wa Masomo nchini Rasilhema kuendendeleza nidhamu na bidii katika kipindi chote watachokuwa masomoni ili kuweza kupata matokeo mazuri katika masomo yao. Hayo yameelezwa wakati wa hafla ya kuwaaga wanafunzi waliopata nafasi ya kuendelea na Masomo ya Digree ya kwanza yaliodhaminiwa na Rasilhema hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mkutano waOfisi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mazizini . Amesema ni vyema wanafunzi hao kuitumia fursa ya udhamini walioipata ya kwenda kusoma nje, kwani kutawasaidia kuengeza elimu ambayo wataweza kuja kuitumia katika kuliendeleza taifa hivyo amewasihi kwenda kuendeleza nidhamu na maadili katika kipindi chote cha masomo yao. Ameeleza kuwa Serikali ya Mapindunzi ya Zanzibar na Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikichukuwa jitihada katika kuhakikisha inaimarisha miundombinu bora kwa wanafunzi ili kuwawezesha kuendelea na elimu ndani na nje ya nchi . Mkurugenzi Mtendaji Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Bw Iddi Khamis Haji amesema wanafunzi 40 walipitia mchakato huo na watano wamebahatika kupata ufadhili huo na wanatarajiwa kuondoka hivi karibuni kwenda kuendelea na masomo ya Chuo Nchini Rasilhema Wanafunzi wanaliopata nafasi hiyo Said Ali Hamadi na Zulfa Rashid Gharib wameipongeza serikali kwa kuibua fursa mbali mbali za masomo nje ya nchi hivyo wameahidi kwenda kusoma kwa bidii ili kuweza kuja kuendeleza taifa