Employers

  1. 1.   Wajibu wa Mwajiri

·       Kila mwajiri anapaswa kuijuilisha Bodi mtumishi mpya anayeajiriwa ndani ya miezi mitatu ili Bodi ijiridhishe kama mwajiriwa huyo ni mdaiwa wa Bodi au la.

·       Ikithibitika kuwa mwajiriwa ni mdaiwa wa Bodi, mwajiri atapaswa kukata kiwango cha deni kutoka kwenye mshahara wa kila mwezi wa mdaiwa kwa utaratibu ambao Bodi itaona unafaa.

·       Mwajiri atawajibika kuwasilisha mikato ya mshahara wa kila mwezi wa mdaiwa si zaidi ya siku 15 za mwezi unaofuata kwa utaratibu utakaotolewa na Bodi.

·       Kwa kukubali kumwajiri mdaiwa wa BMEJZ, mwajiri hatokuwa na nafasi ya kukwepa wajibu wake wa kuanza kukata mshahara wa mdaiwa na kuwasilisha marejesho kwa BMEJZ kwa kisingizio cha kutokuwa mshiriki katika mkataba wa mkopo kati ya BMEJZ na mdaiwa.

  1. 2.   Adhabu kwa Mwajiri Anayekiuka Wajibu Wake

Mwajiri atakayeshindwa kutekeleza wajibu wake ipasavyo anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria zifuatazo:

·          Kutozwa faini au tozo nyengine yoyote ile ambayo Bodi itaona inafaa kwa kuchelewa kuwasilisha kwa wakati mikato ya mshahara wa mdaiwa kwenye ofisi za Bodi (Kifungu cha 27(1) cha Sheria ya Bodi).

·          Kutozwa faini inayofikia shilingi milioni tano au kufungwa jela kwa kifungo kisichopungua miezi 12 au adhabu zote mbili kwa pamoja kwa kushindwa kukata deni la mdaiwa wa Bodi kutoka kwenye mshahara wake na kuwasilisha mikato hiyo kwenye ofisi za Bodi (Kifungu cha 27(2) cha Sheria ya Bodi).

·          Kulipa deni lote linalodaiwa pamoja na tozo nyenginezo ambazo Bodi itaona zinastahiki kulipwa (Kifungu cha 27(3) cha Sheria ya Bodi).