Institutions

  • 1.    Wajibu wa Mdhamini wa Mkopaji

    Mdhamini wa mkopaji anawajibika:

    ·       Kutoa taarifa kwa Bodi kuhusu kumaliza masomo na/au kupata ajira kwa mkopaji.

    ·       Kutoa taarifa sahihi za mkopaji zikiwemo anwani ya makazi, mwajiri au pahala pa kazi endapo mkopaji atakuwa ni mjasiriamali.

    ·       Kumshajiisha mkopaji kulipa deni lake kwa wakati kwa utaratibu uliopangwa na Bodi.

    ·       Kulipa deni endapo mdaiwa atakwepa kulipa deni kwa hiari na kutotekeleza masharti ya marejesho ya mkopo. Aidha, mdhamini au mtu mwengine yeyote (wakala) anaweza kumlipia mkopaji deni lake kwa hiari.

    2.    Adhabu kwa Mdhamini anayekiuka wajibu wake

    Mdhamini atakayeshindwa kutekeleza wajibu wake ipasavyo anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria kama ifuatavyo:

    ·       Kutozwa faini inayofikia shilingi milioni 5 au kufungwa jela kwa kifungo kisichopungua miezi 12 au adhabu zote mbili kwa pamoja kwa kushirikiana na mdaiwa kukwepa kulipa deni analodaiwa. (Kifungu cha 27(2) cha Sheria ya Bodi).

    ·       Kulipa deni lote linalodaiwa pamoja na tozo nyenginezo ambazo Bodi itaona zinafaa kulipwa (Kifungu cha 27(3) cha Sheria ya Bodi).